Sunday, September 9, 2018

NAMNA YA KUPIKA KEKI

NAMNA YA KUPIKA KEKI MAHITAJI: -Mayai sita -Siagi -Sukari (icing sugar) -Baking powder -Unga wa ngano -Mafuta ya kupikia -Flavours za vanilla, choklate au matunda NAMNA YA KUANDAA Chukua mayai yako sita (kwa keki ya ukubwa wa wastani), yagonge kisha chukua siagi (robo kilo) na uiweke kwenye bakuli, ongeza na sukari kwenye siagi kisha mimina mayai kwenye mchanganyiko huo. Koroga mpaka upate uji mzito, unaweza kutumia mashine maalum ya kuchanganyia. Ukishapata uji mzito lakini laini, changanya na unga wa ngano, ongeza baking powder kijiko cha chai kisha weka flavour yoyote unayotaka keki yako iwe, inaweza kuwa vanilla, rose, machungwa, mananasi n.k. Changanya mchanganyiko huo kwa kutumia mwiko kwa dakika mbili mfululizo. Chukua sufuria, ipake mafuta kwa ndani kisha chukua karatasi plain na kuiweka ndani ya sufuria. Mwagia mchanganyiko wako kisha weka kwenye oven na baada ya muda utaanza kusikia harufu nzuri. Ukitaka kujua kama keki yako imeiva, chukua kijiti kikavu na kukiingiza katikati ya keki, kikitoka kikavu basi ujue keki yako imeiva, itoe na iache ipoe, unaweza kuongeza na mapambo unayoyataka, kama kuandika jina au kuweka rangi.

Monday, September 3, 2018

MAPIGANO YAZUKA MJI MKUU WA LIBYA

Serikali ya Libya imetangaza hali ya hatari mara baada ya kuzuka kwa mapigano katika mji mkuu wa nchi hiyo, Tripoli na maeneo yaliyo karibu na mji huo, ambapo watu zaidi ya 39 wamefariki na wengine kujeruhiwa. Libya imetangaza hali hiyo ili kuweza kuwalinda raia wake, mali pamoja na asasi muhimu kwa jamii nzima na wageni wanaoingia nchini humo. Aidha, Serikali hiyo ya Libya imetoa wito wa kusitishwa kwa mapigano hayo na kuheshimiwa kwa makubaliano ya kusitisha uhasama. Hata hivyo, wakati yakitokea hayo, takriban wafungwa 400 wametoroka kutoka gereza moja kusini mwa Tripoli, eneo ambalo pia limeshuhudia mapigano makali katika kipindi cha wiki moja kati ya makundi hasimu.

Friday, August 31, 2018

KUNDI LA PAKA LATIKISA LINDI

Kundi la paka wapatao 12 wameshiriki mazishi ya Salehe Matiko aliyezikwa saa 10 alasiri ya Agosti 24 katika Kijiji cha Chikalala mkoani Lindi. Marehemu Matiko aliuawa kwa kushambuliwa na wakazi wa kijiji hicho kwa tuhuma za ushirikina huku akidaiwa kuwatesa watu ikiwa ni pamoja na kuua ndugu zake. Wananchi wa kijiji hicho walieleza kuchoshwa na kile walichokiita mateso ya Matiko na kuamua kumuwinda na kumshambulia mpaka kupoteza maisha yake. Wakiwa msibani baada ya taratibu zote za kuandaa safari yake ya mwisho, jeneza lake lilibebwa kwa utaratibu wa kawaida lakini ghafla wakiwa barabarani kuelekea makaburini liliibuka kundi la paka lililokuwa likifuata jeneza hilo kwa nyuma hali iliyoibua hofu kwa wanakijiji. Lakini paka hao walifika hadi makaburini ambapo nao walishiriki mazishi yake. Wakati wa kushusha maiti kwenye kaburi lake, paka hao waliinamisha vichwa chini wakionesha utii wao kwa marehemu jambo ambalo liliwashtua wengi. Baada ya kumaliza taratibu zote za kumuhifadhi Matiko watu walioshiriki mazishi hao walitawanyika kama ilivyo ada lakini paka hao hawakutawanyika na badala yake waliendelea kubaki makaburini hapo. Msafiri Msemwa ambaye ni mkazi wa kijiji hicho ameeleza kuwa, waliingia hofu kidogo kwa kuwa sio tukio la kawaida lakini waliendelea na taratibu za mazishi hayo. “Sio jambo la kawaida kutokea ndio maana kila mmoja alikuwa na hofu lakini watu waliendelea kama kawaida mpaka mwisho. “Kila mmoja alikuwa na tafsiri yake kutokana na kundi hilo la paka ambapo muda wote wa mazishi watu walikuwa wakiwatolea macho paka hao huku wakichukua tahadhari kwa lolote ambalo lingeweza kutokea,” amesema

Thursday, August 23, 2018

PILATO NI NANI?

Pontio Pilato Alikuwa Nani? “PILATO alikuwa mtu mwenye dhihaka, mwenye kutilia shaka mambo, na anayewashangaza watu. Watu fulani humwona kuwa mtakatifu, wengine humwona kuwa mtu dhaifu, mwanasiasa aliyekuwa tayari kumdhabihu mtu mmoja ili kuepuka mizozo.”—Pontius Pilate, kitabu kilichoandikwa na Ann Wroe. Uwe unakubaliana na maoni hayo au la, Pontio Pilato alijulikana sana kwa sababu ya jinsi alivyomtendea Yesu Kristo. Pilato alikuwa nani? Tunajua nini kumhusu? Kufahamu vizuri cheo chake kutatusaidia kuelewa matukio muhimu zaidi kuwahi kutukia duniani. Cheo, Kazi, na Mamlaka Maliki Mroma Tiberio alimtawaza Pilato kuwa gavana wa mkoa wa Yudea mwaka wa 26 W.K. Maliwali kama hao walikuwa wanajeshi wa kupanda farasi, yaani, walikuwa na cheo cha chini, wakilinganishwa na watu waliokuwa na vyeo vya juu serikalini. Yaelekea Pilato alijiunga na jeshi akiwa kamanda wa cheo cha chini; kisha akapandishwa cheo hatua kwa hatua; na hatimaye akawekwa rasmi kuwa gavana akiwa na umri usiozidi miaka 30. Pindi fulani, Pilato alivalia mavazi ya kijeshi, yaani, koti la ngozi na bamba la kifuani la chuma. Hadharani alivalia kanzu nyeupe yenye pindo za zambarau. Huenda alikuwa na nywele fupi na alinyoa ndevu zote. Ingawa watu fulani huamini kwamba alitoka Hispania, jina lake linaonyesha alikuwa wa kabila la Pontii, yaani, wakuu wa Wasamnite kutoka kusini mwa Italia. Kwa kawaida maliwali wa cheo cha Pilato walitumwa katika maeneo yasiyostaarabika. Waroma waliona Yudea kuwa mojawapo ya maeneo hayo. Mbali na kudumisha amani, Pilato alisimamia kodi zisizo za moja kwa moja na kodi ya kichwa. Kila siku mahakama za Wayahudi zilishughulikia udumishaji wa haki, lakini kesi zilizohitaji hukumu ya kifo zilipelekwa kwa gavana, ambaye alikuwa na mamlaka kuu zaidi ya kuhukumu. Pilato na mke wake pamoja na waandishi wachache, marafiki na wajumbe kadhaa, waliishi katika jiji la bandarini la Kaisaria. Pilato alisimamia vikosi vitano vya wanajeshi wa kwenda kwa miguu, kila kimoja kikiwa na watu 500 hadi 1,000 na pia wanajeshi 500 wanaopanda farasi. Kwa ukawaida askari wake waliwatundika watu waliovunja sheria. Kulipokuwa na amani, wakosaji waliuawa baada ya kesi kusikilizwa kwa muda mfupi, lakini kulipokuwa na ghasia, waasi waliuawa papo hapo wakiwa wengi. Kwa mfano, Waroma waliwatundika watumwa 6,000 ili kukomesha uasi ulioongozwa na Spartacus. Kulipokuwa na matatizo huko Yudea, kwa kawaida gavana aliwasiliana na mwakilishi wa maliki huko Siria ambaye alisimamia vikosi vya wanajeshi 3,000 hadi 6,000. Hata hivyo, kwa muda mwingi ambao Pilato alikuwa gavana, hakukuwa na mwakilishi huko Siria na hivyo Pilato alilazimika kukomesha ghasia upesi. Kwa kawaida, magavana waliwasiliana na maliki. Mambo yaliyohusu cheo chake au tisho lolote kuelekea utawala wa Roma lilipaswa kuripotiwa kwa maliki, kisha sheria za kifalme zingetungwa. Yaelekea gavana alijitahidi kumweleza maliki mambo yanayohusu mkoa wake kabla ya watu kulalamika. Matatizo yalipoanza huko Yudea, Pilato alikuwa na wasiwasi sana. Mbali na masimulizi ya Injili, wanahistoria Flavio Yosefo na Philo ndio walioandika mambo mengi kumhusu Pilato. Pia, mwanahistoria Mroma, Tasito alieleza kwamba Pilato alimuua Christus, ambaye Wakristo wanaitwa kwa jina lake. Hasira ya Wayahudi Yachochewa Yosefo anasema kwamba kwa sababu ya sheria ya Wayahudi iliyopinga kutengeneza sanamu, magavana Waroma hawakupeleka huko Yerusalemu bendera za kijeshi zilizokuwa na sanamu za maliki. Kwa kuwa Pilato hakuheshimu sheria hiyo, Wayahudi wenye hasira walipeleka malalamiko yao Kaisaria. Kwa siku tano, Pilato hakuchukua hatua yoyote. Siku ya sita, akawaamuru askari wake wawazingire walalamikaji na kutisha kuwaua iwapo hawatatawanyika. Wayahudi waliposema kwamba afadhali wafe kuliko kuona Sheria yao ikivunjwa, Pilato alitulia na kuamuru sanamu hizo ziondolewe. Pilato hakujizuia kutumia nguvu. Katika kisa kimoja kilichoandikwa na Yosefo, Pilato alianzisha mradi wa kutengeneza mfereji wa kuleta maji Yerusalemu na kuendeleza mradi huo kwa kutumia pesa za hazina ya hekalu. Pilato hakuchukua pesa hizo waziwazi, kwa kuwa alijua kwamba ni kukufuru kupora hekalu, na hilo lingewafanya Wayahudi wenye hasira wamwombe Tiberio amfute kazi. Hivyo, yaelekea Pilato alishirikiana na wasimamizi wa hekalu. Pesa zilizowekwa wakfu, zilizoitwa “korbani” zingeweza kutumiwa kihalali kufanya kazi ambazo zingewanufaisha wakaaji wa jiji. Lakini maelfu ya Wayahudi walikusanyika kuonyesha ghadhabu yao. Pilato aliwaagiza askari wachangamane na umati, naye akawaamuru wasitumie upanga bali wawapige walalamikaji kwa rungu. Yaelekea alitaka kuudhibiti umati bila kuchochea mauaji. Inaonekana alifaulu, ingawa watu kadhaa walikufa. Huenda watu waliomwambia Yesu kwamba Pilato alichanganya damu ya Wagalilaya na dhabihu zao walikuwa wakirejelea tukio hilo.—Luka 13:1. “Kweli Ni Nini?” Pilato alijulikana kwa sababu ya uchunguzi aliofanya kuhusu mashtaka ya makuhani wakuu Wayahudi na wanaume wazee yaliyosema kwamba Yesu alijifanya kuwa Mfalme. Aliposikia kwamba Yesu alikuja kutoa ushahidi kwa ajili ya ile kweli, Pilato aliona kwamba mfungwa huyo hakuwa tisho kwa Roma. “Kweli ni nini?” akauliza, akifikiri kwamba kweli ni wazo lisiloweza kueleweka na halihitaji kufikiriwa sana. Alikata kauli gani? “Mimi sioni uhalifu wa mtu huyu.”—Yohana 18:37, 38; Luka 23:4. Huo ungekuwa mwisho wa kesi ya Yesu, lakini Wayahudi walisisitiza kwamba alikuwa analipindua taifa. Wivu ndio uliowafanya makuhani wakuu wamshtaki Yesu, na Pilato alijua hivyo. Pia, alijua kwamba kumwachilia Yesu kungeleta shida, na alitaka kuepuka jambo hilo. Tayari kulikuwa na matatizo mengi, kwa kuwa Baraba na wengine walikuwa kifungoni kwa shtaka la uchochezi na mauaji. (Marko 15:7, 10; Luka 23:2) Isitoshe, mizozo iliyokuwa imetokea kati ya Pilato na Wayahudi ilikuwa imemharibia sifa mbele ya Tiberio aliyejulikana kwa kuwachukulia hatua kali magavana wabaya. Hata hivyo, kukubaliana na Wayahudi kungeonyesha udhaifu. Hivyo, Pilato hakujua la kufanya. Baada ya kujua Yesu alitoka eneo gani, Pilato alijaribu kutuma kesi hiyo kwa Herode Antipa, mtawala wa wilaya ya Galilaya. Hilo lilipokosa kufaulu, Pilato alijaribu kuwashawishi watu waliokusanyika nje ya nyumba yake waombe Yesu aachiliwe kulingana na desturi yake ya kumfungulia mfungwa mmoja wakati wa Pasaka. Umati ulipaaza sauti ukimtaka Baraba.—Luka 23:5-19. Huenda Pilato alitaka kufanya lililo sawa, lakini alitaka pia kutetea cheo chake na kuupendeza umati. Mwishowe, badala ya kusikiliza dhamiri yake na kufuatia haki, alitanguliza kazi yake. Aliomba maji, akanawa mikono na kudai kwamba hakuwa na hatia kwa kifo ambacho aliamuru.* Ingawa alijua kwamba Yesu hakuwa na hatia, Pilato aliagiza apigwe mijeledi na kuwaruhusu askari-jeshi wamdhihaki, wampige, na kumtemea mate.—Mathayo 27:24-31. Pilato alijaribu kwa mara ya mwisho kumwachilia Yesu, lakini watu wakapaaza sauti kwamba akimfungua, yeye si rafiki ya Kaisari. (Yohana 19:12) Pilato aliposikia hivyo, alifanya walivyotaka. Msomi mmoja alisema hivi kuhusu uamuzi wa Pilato: “Suluhisho ni rahisi: muue mtu huyo. Kinachopotea tu ni uhai wa Myahudi mmoja ambaye anaonekana kuwa hana maana yoyote; ungekuwa upumbavu kusababisha ghasia kwa sababu yake.” Ni Nini Kilichompata Pilato? Tukio la mwisho lililorekodiwa kuhusu maisha ya Pilato lilihusu mapambano. Yosefo anasema kwamba Wasamaria wengi wenye silaha walikusanyika kwenye Mlima Gerizimu wakitaka kufukua hazina ambazo walidhani zilizikwa huko na Musa. Pilato aliingilia kati, na majeshi yake yakawaua watu kadhaa. Wasamaria walipeleka malalamiko yao kwa Lusio Vitelio, gavana wa Siria aliyekuwa na cheo cha juu kuliko Pilato. Hatujui iwapo Vitelio aliona kwamba Pilato alikuwa amepita mipaka. Hata hivyo, alimwamuru Pilato aende Roma kujibu mashtaka hayo mbele ya maliki. Lakini kabla ya kufika huko, Tiberio akafa. “Baada ya hapo, Pilato hatajwi tena katika historia ila katika hekaya mbalimbali,” lasema gazeti moja. Lakini watu kadhaa wamejaribu kueleza zaidi. Imedaiwa kwamba Pilato alibadilika akawa Mkristo. “Wakristo” wa Ethiopia wanamwona kuwa “mtakatifu.” Eusebio, aliyeandika mwishoni mwa karne ya tatu na mwanzoni mwa karne ya nne, alikuwa wa kwanza kati ya wengi kusema kwamba Pilato alijiua kama Yuda Iskariote. Hata hivyo, hakuna anayejua kwa hakika kilichompata Pilato. Yaelekea Pilato alikuwa mkaidi, asiyejali, na mkandamizaji. Hata hivyo, tofauti na maliwali wengi wa Yudea ambao walikuwa na cheo hicho kwa muda mfupi, Pilato alikuwa gavana kwa miaka kumi. Kwa maoni ya Waroma, Pilato alikuwa gavana hodari. Ametajwa kuwa mtu mwoga ambaye alikuwa na hatia ya kuruhusu Yesu ateswe na kuuawa ili ajifaidi. Wengine wanasema kwamba kazi ya Pilato haikuwa kutetea haki bali ilikuwa kudumisha amani na hali njema ya Waroma. Siku za Pilato zilikuwa tofauti sana na zetu. Hata hivyo, hakuna hakimu anayefuata haki anayeweza kumhukumu mtu ikiwa anamwona kuwa hana hatia. Kama Pontio Pilato hangekutana na Yesu, jina lake halingekuwa maarufu sana. C n P By Jumong S Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Likes:Sakasaka Mao, kilwakivinje, Lukataluko and 2 others Mega Mind Nyerere JF-Expert Member Yesterday at 6:34 AM #2 Kumbe huyo kwenye picha ndiye Pilato. Mbona hata hatishi Like Quote Reply Report Likes:mtu chake, The Icebreaker, Eminem jr and 2 others MLALE Senior Member Yesterday at 6:39 AM #3 Poncio Pilato Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Ras Jeff Kapita JF-Expert Member Yesterday at 6:44 AM #4 Safi sana mkuu tunashukuru kwa kutuwekea strue story mahususi ya mtu huyu Like Quote Reply Report Likes:Eminem jr MarkHilary JF-Expert Member Yesterday at 6:46 AM #5 Huyu jamaa alikua na hekima Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Likes:Eminem jr Jumong S JF-Expert Member Yesterday at 6:46 AM #6 ras jeff kapita said: Safi sana mkuu tunashukuru kwa kutuwekea strue story mahususi ya mtu huyu Pamoja sana rafiki. Warumi walikuwa vzr kimfumo wa serikali. Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Likes:ras jeff kapita Baba_Enock JF-Expert Member Yesterday at 6:47 AM #7 Pirato??? GPA ya 32 Like Quote Reply Report Likes:The Icebreaker K Kibuyu180 JF-Expert Member Yesterday at 7:02 AM #8 Safi na Hongera mkuu Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Monde Arabe JF-Expert Member Yesterday at 7:04 AM #9 Safi sana! Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Da'Vinci JF-Expert Member Yesterday at 7:05 AM #10 Hingera kwa mada nzurii Like Quote Reply Report Likes:Eminem jr U Undertwentyboy JF-Expert Member Yesterday at 7:30 AM #11 nilianza kukuelewa ila nivoiona picha ya pilato nimekua na mashaka kuwa unatulisha matango pori ya misri pilato na camera wapi na wapi mkuu Like Quote Reply Report Likes:jogi, dolevaby and mtu chake Eminem Jr JF-Expert Member Yesterday at 7:37 AM #12 Asante kwa kutuelewesha maana jamaa tulikuwa tunamuelewa juu juu tu Like Quote Reply Report E Edson Silumbe Member Yesterday at 7:47 AM #13 Simulizi nzuri Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Kelao JF-Expert Member Yesterday at 7:50 AM #14 Story ya kweli ila picha sio Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Likes:dolevaby and mtu chake Elli JF-Expert Member Yesterday at 7:52 AM #15 Asante sana Mpwa, sasa nitakua napata picha ya Mhusika "Akateswa zamani za Pontio Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, siku ya tatu akafufuka kutoka kwa Wafu, akapaa mbinguni..." Like Quote Reply Report Likes:Jumong S and mtu chake Wilbald JF-Expert Member Yesterday at 7:54 AM #16 Haliitwi bamba la kuvalia kifuani...inaitwa dirii Like Quote Reply Report Likes:jogi and Nuhu39 Mtu Chake JF-Expert Member Yesterday at 7:56 AM #17 Ndio huyo ktk picha? Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report Mtemi Mpambalioto JF-Expert Member Yesterday at 8:07 AM #18 Mega Mind Nyerere said: Kumbe huyo kwenye picha ndiye Pilato. Mbona hata hatishi haha pilato kapiga picha HD! au zaman kulikuwa na mikamera ya hivo! Like Quote Reply Report Kisikiji JF-Expert Member Yesterday at 8:08 AM #19 Mkuu kwenye picha tutake radhi, isije kutuaminisha kama baadhi wanavyoamini ya Yesu na kuiabudu. Like Quote Reply Report Likes:Nuhu39 Nuhu39 JF-Expert Member Yesterday at 8:17 AM #20 Alikuwa na busara katika uongozi wake. Sent using Jamii Forums mobile app Like Quote Reply Report 1 2 Next Share: Facebook Twitter Google+ Reddit WhatsApp Email Link Telegram Instagram Remove formatting Bold Italic Underline Text color Font size Insert link Insert image Smilies Insert Alignment List Undo Redo Toggle BB code Write your reply... POST REPLY PREVIEW ATTACH FILES Edit avatar sumbi fabian New Member Messages 3 Likes 0 Trophy points 3 FORUM STATISTICS THREADS 1,192,801 MEMBERS 452,071 POSTS 27,746,863 FACEBOOK TWITTER TELEGRAM INSTAGRAM Habari na Hoja mchanganyiko Previous WHO WE ARE JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic. You are always welcome! Read more... WHERE ARE WE? We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually. For anything related to this site please Contact us. Contact us now... DISCLAIMER JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users.. Read more... FORUM RULES JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you. You MUST read them and comply accordingly. Read more... PRIVACY POLICY We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one. Read our Privacy Policy. Proceed here... Next Contact usTerms and rulesJamiiForums' Privacy PolicyHelp Up to top

Saturday, August 11, 2018

KITU CHA KWANZA ALICHOKISEMA RICH MAVOKO BAADA YA KUSHINDA KESI DHIDI YA WBC

Baada ya kushinda kesi dhidi ya uongozi aliokuwa nao kwanza wa WCB ambapo kesi hiyo ilienda kusikilizwa katika ofizi za BASATA  nakuoneka kuwa Rich mavoko alisainishwa mkataba ulikuwa ukimkandamiza yeye pamoja na muziki wke kwa mara ya kwanza msnii huyo ametoa ujumbe mzito alkini wa kuishukuru BASATA kwa kumsaidia kutoka huko. Katika ukurasa wake wa instagram, Rich mavoko aliandika “Nimejifunza vingi lakini kikubwa ni umhimu wa kukaa karibu na walezi wetu maana changamoto ni nyingi, na kuna mengi lakini yote mnaweza kuyajua kama tukiwa karibu na nyie, leo mmenipa maana ya neno mama ni mama hata kama akiwa kilema, hata iweje nyie ndio walezi wa sanaa yetu.” Tangu kumekuwa na tetesi za Rich Mavoko kutoka katika lebel hiyo hakuwahi kuzungumza kitu chochote mpaka hapo alipomaliza kesi  hiyo na kuanza kuonekana kwa habari hiyo katika vyombo vya habari.

Friday, August 10, 2018

MAHAKAMA YAAMURU KUONDOLEWA ZACHARIA NA LAUWO KATIKA KESI INAYOMKABIRI ALIYEKUWA MWENYEKITI NA MAKAMU MWENYEKITI WA SIMBA SC

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa siku saba kwa upande wa jamhuri kukamilisha mchakato wa kubadilisha hati ya mashtaka ili kuwaondoa washtakiwa wawili katika kesi inayomkabili aliyekuwa Rais wa Klabu ya Simba SC, Evans Aveva na Makamu wake, Godfrey Nyange maarufu Kaburu au kuifuta kesi hiyo. Washtakiwa wanaotakiwa kuondolewa katika kesi hiyo ni Zacharia Hans Poppe na Frank Lauwo ambao hawajawahi kufika mahakamani hapo. Akitoa uamuzi huo leo mahakamani hapo,  Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amesema bado wanaifuatilia kesi hiyo kwa ukaribu lakini itafika mahali uvumilivu utawashinda na kama jamhuri wameshindwa basi waifute. Mahakama imeamuru Zacharia Hans Poppe (kulia) aondolewe kwenye kesi ya viongozi wa Simba SC “Ukiangalia afya ya Aveva unaona kabisa ni mgonjwa, anatakiwa kwenda kliniki kwa wiki mara mbili, hivyo basi tunalazimika kuangalia ratiba ya matibabu yake ili tupange kesi,” amesema Hakimu Simba. Awali, Wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai ameieleza mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa, kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na tayari wameshaifanyia marekebisho hati ya mashtaka na kwamba wanasubiri kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) ili kesi hiyo iendelee kwa mujibu wa sheria. Baada ya Wakili huyo kudai hayo, Aveva aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe za karibu za kusikiliza kesi hiyo kwa madai kuwa imechukua muda mrefu huku Wakili wa Jamhuri Shadrack Kimaro na Wakili Takukuru, wamekuwa wakirushiana mpira. Kwa upande wake Kaburu ambaye ni mshtakiwa wa pili amedai kuwa ni zaidi ya mwaka mmoja sasa umepita wako mahabusu tangu kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani hapo huku mawakili hao wakidai faili liko kwa DPP. Alidai mshtakiwa wa kwanza, Aveva ana matatizo ya kiafya na kwamba kila wiki anaenda kliniki kwa ajili ya matibabu hivyo basi kuendelea kurushiana mpira ni kuwaumiza na kwamba hadhani kama DPP ameshindwa kushughulikia kesi yao, bali ni ucheweshaji wa makusudi unaofanywa na mawakili hao katika kesi hiyo kutoka kwa DPP na Takukuru. Amedai upelelezi umeshakamilika kilichobaki ni kubadilisha hati hiyo ili kesi ianze kusikilizwa, hivyo basi anaiomba mahakama hiyo kupanga tarehe za karibuni ili waweze kuwaona na kuwaonea huruma kuliko kupanga tarehe za mbali za wiki mbili. Wakili Swai alidai kuwa, hoja zilizotolewa na washtakiwa hao zina mashiko na kuahidi kushughulikia suala hilo. Hakimu Simba alihairisha kesi hiyo had I Agosti 17 mwaka huu. Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka kumi likiwemo la kula njama, matumizi mabaya na kughushi nyaraka ikionyesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa Dola za Marekani 300,000 kwa Aveva kitu ambacho si kweli. Wanadaiwa, kuwa  Machi 10 na 16, 2016, Aveva na Nyange waliandaa nyaraka za kuhamisha dola za kimarekani 3000,000 kutoka kwenye akaunti ya klabu ya Simba kwenda kwenye akaunti ya Aveva wakijua kuwa wanachofanya ni kosa.

Monday, August 6, 2018

MDHAMINI MPYA SIMBA SC KUJENGA UWANJA WA BUNJU

PAMOJA na kutambulisha jezi zake mpya za msimu ujao, klabu ya Simba imeingia mkataba wa mwaka mmoja na Kampuni ya A1 Products kupitia kinywaji cha Mo Energy Drink wenye thamani ya Sh. Milioni 250.Kaimu Rais Simba SC, Salim Abdallah 'Try Again' amesema fedha hizo zitaenda katika mradi wa ujezi wa Uwanja mpya wa klabu huko Bunju.

SIMBA SC IMETAMBULISHA JEZI MPYA

Mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba SC wametambulisha jezi zao mpya zitakazotumia msimu wa 2018/19. Kwamujibu wa Mkuu wa habari na mawasiliano wa Simba, Haji Manara amesema kuwa jezi hizo zitaanza kuuzwa rasmi hapo kesho kuanzia majira ya saa 10: 00 alasiri. Simba wamezitangaza jezi hizo ambazo zitatumika kwenye michezo mbalimballi. Wakati jezi zao nyeupe zitakuwa kwaajili ya mechi za ugenini huku nyekundu zikitumika kwa mechi za ugenini. Simba imetambulisha jezi hizo zenye nembo ya mdhamini mkuu SportPesa na Mo Energy Drink ambao ni wadhamini wapya waliotangazwa leo kwa kuingia mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi milioni 250.

Friday, August 3, 2018

UFAFANUZI WA TFF JUU YA ALIKIBA

Mchezaji mpya wa Coastal Union ya Tanga, Ally Salehe Kiba ‘Ali Kiba’. BAADA ya hivi karibuni baadhi ya watu kudai kuwa mchezaji mpya wa Coastal Union ya Tanga, Ally Salehe Kiba ‘Ali Kiba’ kuwa kanuni za Ligi Kuu Bara hazimruhusu kuitumikia timu hiyo katika ligi hiyo, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetoa msimamo wake. Ilidaiwa kuwa kanuni za ligi kuu hazimruhusu Kiba kuitumikia Coastal katika ligi hiyo kwa sababu ni mwanamuziki jambo ambalo lilizua maswali mengi kwa baadhi ya wapenzi na mashabiki wa soka hapa nchini. Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Salum Madai ameliambia Championi Ijumaa kuwa, hakuna kanuni yoyote inayomzuia Ali Kiba asiitumikie Coastal Union katika michuano ya kwa sababu tu ni mwanamuziki. Alisema mchezo wa soka haubagui, kila mtu anaruhusiwa kucheza. “Kanuni zetu hazijasema mchezaji lazima awe na kazi moja tu, anaweza kuwa mcheza mieleka, mcheza kikapu na mchezaji wa soka la ufukweni na kusajiliwa kucheza soka. “Kwa hiyo, Coastal Union wao kama wameona kuwa Ali Kiba anaweza kuwasaidia hiyo ni juu yao ila hakuna kanuni inayomzuia kutoitumikia timu hiyo kwa sababu ya kazi yake,” alisema Madadi.

Wednesday, August 1, 2018

ALIKIBA KUIKOSA MECHI YA UFUNGUZI WA LIGI

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na ngoma yake ya ‘Mvumo wa radi’ Ali Kiba amedaiwa anaweza akakosa mechi muhimu kabisa ndani ya Coastal Union. Ali Kiba ambaye alitangazwa kusajiliwa na timu hiyo ya mkoani Tanga wiki iliyopita, anasemekana kuwa ana aweza akakosa mechi yake ya kwanza ndani ya timu hiyo kutokana na shoo yake ya muziki. Ligi Kuu imepangwa kuanza kutimua vumbi Agosti 22 lakini ratiba ya shoo ya Alikiba inaonyesha itaanza Agosti 17, 18 na 25, mwaka huu huko Toronto, nchini Canada katika shoo iliyopewa jina la The All Star Music. Ratiba inaonyesha Coastal Union wataanza ligi, Agosti 22 dhidi ya Lipuli FC kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga hivyo Alikiba hatokuwa sehemu ya wachezaji watakaocheza mechi hiyo. Meneja wa Coastal Union, Said Hilal ameweka wazi kuwa wanatambua majukumu ya kimuziki ya Ali Kiba hivyo hawana tatizo juu ya kukosa kwake mechi. Tunajua AliKiba ana majukumu yake mengi na sisi kama klabu hatuwezi kumzuia kwenye hilo pale ambapo atakuwepo atafanya kazi na wenzake hivyo hakuna tatizo”.

Tuesday, July 31, 2018

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA LEO

Tetesi za Usajili barani Ulaya leo 31.7.2018 Real Madrid haina mpango wa kumsajili mchezaji wa safu ya kati wa Chelsea Willian, mwenye umri wa miaka 29, na wanaemtaka tu ni mlinda lango wa Ubelgiji Thibaut Courtois, mwenye umri wa miaka 26, kutoka the Blues. (marca)  Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Willian anasema ni mwenye ”furaha sana katika Chelsea na anafurahia kuishi London. (Globo Esporte, via Mirror) Meneja wa Leicester Claude Puel amesisitizia tena imani yake kwamba mlinzi wa England Harry Maguire mwenye umri wa miaka 25 – anayechezea Manchester United – atasalia na the Foxes katika msimu mpya. (Sky Sports) Maguire anatarajiwa kupewa donge nono katika mkataba wake mpya na Leicester na hivyo kuongezewa malipo yake ya wiki kutoka £50,000 hadi £95,000. (Mirror) Everton wako mstari wa mbele katika harakati za kusaini mkataba na Mchezaji wa safu ya mashambulizi wa Manchester United na Argentina Marcos Rojo, mwenye umri wa miaka 28 ambae aliambiwa anaweza kuondoka kama tahamani yake ya £30m itatimizwa. (Mirror) Liverpool wanajiamini kuwa wao ndio watakao saini mkataba na mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane, mwenye umri wa miaka 26, kwa mkataba wa muda mrefu mnamo wiki zijazo. (Mirror) Wakati huo huo , mchezaji wa the Reds kutoka Ubelgiji Divock Origi, 23, anasakwa kwa deni na Besiktas pamoja na Fenerbahce.(Talksport) The Blues wanaangalia uwezekano wa Kumnunua mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal kutoka Wales -Aaron Ramsey Chelsea wamekuwa na mazungumzo ya wazi na Inter Milan juu ya mchezaji wao wa safu ya kati , raia wa Uruguay Matias Vecino, mwenye umri wa miaka 26, na wakatoa £35.5m kwa Juventus ili wamchukue Muitaliano Mattia Caldara mwenye umri wa miaka anayecheza safu ya ulinzi katika timu ya taifa ya Italia. (London Evening Standard) The Blues pia wanaangalia uwezekano wa Kumnunua mchezaji wa kiungo cha kati wa Arsenal kutoka Wales -Aaron Ramsey, mweney umri wa miaka 27 kwa £30m (Telegraph) Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri anasema lengo lake kuu ni kumpata mshambuliaji wa Buyern Munich Robert Lewandowski, Lazio amembiwa na the Gunners kuwa lazima walipe £7m ikiwa wanataka kusaini mkatapa na mchezaji wa safu ya mashambulizi Muhispania Lucas Perez. (Talksport) Newcastle wana nia ya kumchukua Nicolas Tagliafico wa Ajax na mchezaji wa kimataifa wa Argentina , lakini gharama ya £8m na madai ya mchezaji huyo wa safu ya nyuma kushoto mwenye umri wa miaka 23 huenda yakawa zaidi ya bajeti iliyopo ya meneja wa Magpies Rafael Benitez. (Newcastle Chronicle) Yanga wafanya Maamuzi haya kwa Rostand Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri amemtaja mchezaji wa Bayern Munich na mshambuliaji wa Poland Robert Lewandowski, mwenye umri wa miaka 29, kuwa ndiye mchezaji anayemlenga zaidi kumnunua (Star) Brighton imekubali kumuuza mshambuliaji wa England Sam Baldock mwenye umri wa miaka 29- kwa Reading. (Argus) Mourinho amewasihi wachezaji kama Paul Pogba, Romelu Lukaku na Jesse Lingard wapunguze mapumziko yao wawasaidie wachezaji kwenye timu zao wasio na uwezo Leicester itakubali malipo ya £18m kumnunua mshambuliaji kutoka Algeria Islam Slimani, lakini hatma ya siku zijazo ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 haijaamliwa mpaka mwishoni mwa Agosti wakati msimu wa uhamisho utakapomalizi (Leicester Mercury) Meneja wa Paris St-Germain Thomas Tuchel amekataa kuingizwa kwenye taarifa za uvumi zinazokihusisha kilabu na uhamisho wa mchezaji wa Chelsea na ttimu ya Ufaransa wa safu ya kati N’Golo Kante, mwenye umri wa miaka 27. (Talksport) Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amewatolea wito wachezaji kama vile Paul Pogba, Romelu Lukaku na Jesse Lingard, wote wakiwa na umri wa miaka 25, kupunguza mapumziko yao ili kuwasaidia wachezaji katika timu zao wenye uwezo mdogo ambao wameshindwa kufanikiwa kucheza mchezo wa kuridhisha katika kipindi cha kabla ya msimu (Times – subscription required) Mchezaji wa England anayeichezea kikosi cha Middlesbrough cha vijana walio chini ya miaka 21 kwa sasa Patrick Bamford, mwenye umri wa miaka 24, yuko karibu kuhamia kwa mahasimu wao katika Ligi ya Championi Leeds United kwa gharama ya awali ya awali ya kanda ya £7m. (Guardian) Wakati huo huo , Boro wamekataa pendekezo la Wolves ambao ni wageni katika Premier League ya kumchukua winga wao Adama Traore mwenye umri wa miaka 22 . (Express & Star) Mchezaji wa kiungo cha kati wa Morocco Younes Belhanda, anayeichezea Crystal Palace, amemua kuwa hatahamia England na kijana huyo mwenye umri wa miaka 28 anasisitiza kuwa anafurahia kuwa Galatasary Turkish. (Football.London) Mchezaji wa safu ya kati wa Paris St-Germain Mfaransa Adrien Rabiot, mwenye umri wa miaka 23, anakaribia kusaini mkataba na Ligue 1 champions. (ESPN) Mlinzi wa Everton Matty Pennington analengwa na Leeds – ambako alikuwa katika msimu uliopita kwa deni na Wigan pia wanamtaka Muingereza huyo mwenye umri wa miaka 23.. (Liverpool Echo) Kocha wa zamani wa walinda lango Kevin Hitchcock ameteuliwa kufanya kazi hiyo hiyo katika timu ya Super Ligi ya India ya Chennaiyin FC -akijiunga na meneja wa zamani wa Aston Villa John Gregory. (Birmingham Mail)

Sunday, July 29, 2018

NYOTA YA MBWANA SAMATTA YAZIDI KUNG'ARA

NAHODHA wa timu ya Taifa Stars, Mbwana Samatta, amezidi kuziumiza vichwa baadhi ya timu kubwa barani Ulaya baada ya Borussia Dortmund, inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ujerumani maarufu Bundesliga, kuihitaji saini yake. Tayari Levante inayoshiriki Ligi Kuu nchini Hispania ‘La Liga’ imeshaweka mezani Euro milioni 4 ili kuinasa saini ya Mtanzania huyo huku timu yake ya Genk ya Ubelgiji, ikisema kiasi hicho cha fedha ni kidogo kulinganisha na uwezo wa mchezaji wao. Meneja wa Samatta, Jamal Kisongo alisema Dortmund pamoja na Metz ya Ufaransa nazo zinaitaka huduma ya Samatta japo Levante ndio walioko kwenye kasi kubwa. “Licha ya kwamba Levante ndio wameenda rasmi lakini hata Borussia (Dortmund) na Metz, nao wameonyesha nia ya kuitaka saini yake, nadhani muda sio mrefu kila kitu kitakuwa wazi,” alisema. Kama Dortmund watafika bei inamaanisha Samatta atakwenda kugombania namba na akina Shinji Kagawa na Mario Gotze. Katika hatua nyingine Samatta leo anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kitakachowakabili Lokeren, mchezo wao wa ufunguzi Ligi Kuu nchini Ubelgiji. Msimu mpya wa ligi nchini humo umeanza juzi Ijumaa na Genk ya Samatta, wao wanaianza safari yao ya kuusaka ubingwa leo ugenini dhidi ya wapinzani wao hao Uwanja wa Daknamstadio. Baada ya mchezo huo wa ligi, kikosi hicho cha Genk kitakuwa na kazi nyingine Jumatano kucheza na Fola Esch mchezo wa marudiano kutafuta tiketi ya kufuzu michuano ya Europa League. Genk wamejiweka kwenye mazingira mazuri ya kufuzu kwani mchezo wa kwanza timu hizo zilipokutana katikati ya wiki hii, kikosi hicho cha akina Samatta kilishinda mabao 5-0 nyumbani

Friday, July 27, 2018

AHADI YA KOREA KASKAZINI KWA MAREKANI YAANZA KUTEKELEZWA

Korea Kaskazini yarejesha mabaki ya Wamarekani waliokufa vitani  Korea Kaskazini yarejesha mabaki ya Wamarekani waliokufa vitani Korea Kaskazini imeanza kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano kati ya Rais Donald Trump na kiongozi wao, Kim Jong-un kwa kurejesha mabaki ya wanajeshi wa Marekani waliokufa kwenye ardhi ya nchi hiyo. Nchi hiyo imeripotiwa kukabidhi kwa jeshi la Marekani mabaki ya maelfu ya waliokuwa wapiganaji wa Marekani waliokufa kwenye vita kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini, mwaka 1950-1953. Ndege ya jeshi la Marekani imefanya safari kadhaa kwenye Pwani ya Korea Kaskazini na kubeba mabaki hayo ambayo yamepelekwa nchini Korea Kusini. Kim Jong-un alimuahidi Trump kuwa atakabidhi mabaki hayo walipokutana nchini Singapore; na hii imekuwa ahadi ya kwanza inayoonekana kutekelezwa kwa kiwango cha asilimia 100. Ikulu ya Marekani imeelezwa kufurahishwa na hatua hiyo ya Korea Kaskazini. “Leo Kim Jong-un ametekeleza sehemu ya ahadi yake aliyompa Rais Trump kurejesha mabaki ya wapiganaji wetu. Tumetiwa moyo na hatua iliyochukuliwa na Korea Kaskazini kwa ajili ya mabadiliko chanya,” imeeleza taarifa hiyo. Kwa mujibu wa ratiba, Agosti 1 mwaka huu wanajeshi wa Marekani watatoa heshima zao kwa mabaki ya wapiganaji hao katika eneo la kijeshi la Osan nchini Korea Kusini. Habari kubwa katika Magazeti ya Tanzania leo Julai 27, 2018 Takribani wanajeshi 7,700 wa Marekani wanatajwa kupoteza maisha kwenye vita ya Korea Kaskazini na Korea Kusini, katika miaka ya 1950. Mabaki ya askari 5,300 wa Marekani yalikuwa kwenye ardhi ya Korea Kaskazini. Katika vita hiyo mbaya kuwahi kutokea kwenye eneo hilo, mamilioni ya watu walipoteza maisha ikiwa ni pamoja na wanajeshi 36,000 wa Marekani.

KUPATWA KWA MWEZI

  Leo usiku Watanzania kushuhudia tukio refu zaidi la kupatwa kwa mwezi katika historia, Kama umefanikiwa kuiona Ijumaa ya leo Julai 27, 2018 basi mshukuru Mungu sana kwani umepata bahati ya kushuhudia tukio kubwa la kupatwa kwa mwezi usiku wa leo.  Kwa mujibu wa maelezo kutoka kwenye Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) tukio hilo litatokea majira ya kuanzia saa 4:30 usiku hadi 6:14 . Tukio la kupatwa kwa mwezi linatarajiwa kuonekana vizuri katika maeneo mengi ya bara la Afrika, Asia na Ulaya. Hapa nchini Tanzania tukio hilo linatarajiwa kuonekana katika maeneo mengi na linatarajiwa kudumu kwa takribani masaa mawili. Kupatwa kwa Mwezi hutokea wakati Dunia, Mwezi na Jua vinapokuwa kwenye mstari mmoja. Hali hiyo inapotokea mwanga wa jua unaofika katika uso wa mwezi huzuiwa na duara la Dunia. Katika mpangilio huo nuru ya Mwezi huonekana kuwa na giza (Total Lunar Eclipse), hali inayotarajiwa kujitokeza katika maeneo ya bara la Afrika, Asia na Ulaya usiku wa leo tarehe 27 Julai 2018. Kupatwa kwa Mwezi husababisha mabadiliko katika nuru ya mwezi na hivyo kufanya nuru ya mwezi kuwa hafifu(Partial Lunar Eclipse) au kuwa giza (Total Lunar Eclipse). Kwa kuwa kupatwa kwa mwezi kutatokea kipindi Mwezi ukiwa mbali zaidi na Dunia, inatarajiwa kuwa tukio hili litaonekana kwa muda mrefu zaidi ukilinganisha na matukio mengine katika karne ya 21.

Tuesday, July 24, 2018

TETESI ZA USAJILI COASTAL UNION

Kiukweli siku zimebaki kidogo lakini na sisis kama zoezi letu limefikia ukingoni nafikiri mpaka kesho tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kueleza nani na nani tumemsajili. Kwa sababu kwa sasa ndiyo tunamalizia watu wengine maswala ya mikataba sasa sirahisi kuweza kumtaja mkataba bado haja saini mwisho wasiku anaweza akageuza nia na ikawa kitu kingine. Kwa kiasi kidogo kuna ukweli wa kutaka kumsaini Alikiba lakini pia mambo haya jakaa sana sawa lakini wenyewe mnamuona naye ni mchezaji ingawaje si wa kiwango cha juu kwasababu hana mazoezi ya mara kwa mara ya kucheza mpira hivyo kuwa katika mazungumzo ni kweli. Alikiba ataweza kuisaidia Coastal Union licha ya uchezaji ndani ya uwanja lakini pia ataweza kuibeba klabu hiyo kupitia umaarufu wa staa huyo wa muziki nchini na bara zima la Afrika. Klabu ya Coastal Union imepanda rasmi ligi kuu mwaka huu baada ya kuiyaga michuano hiyo msimu wa mwaka 2015/16.

Saturday, July 21, 2018

THIS IS SIMBA

Usajili mwingine uliokamilika usiku wa Jana Simba huu hapa   - July 21, 2018 . Usajili mwingine uliokamilika  Ukisikia Simba hawatanii hawatanii kweli na wamekuwa tayari kufanya lolote linapokuja suala la Kumuhitaji mchezaji mzuri ambaye wanaamini anaweza Kuwasaidia kwenye Kikosi chao kwaajili ya ligi Kuu na mashindano mengine kitaifa na Kimataifa ambayo watashiriki. Simba siku ya Jana wamefanikiwa kumnasa Kiungo mzambia Chama Clatous kutoka katika Klabu ya Dynamos Fc ya Huko nchini Zambia.

Friday, July 20, 2018

WEMA SEPETU AACHIWA HURU

   BREAKING: Wema aachiwa huru na mahakama, Wakili wake awaonya wasanii juu ya matumizi ya madawa ya kulevya (+video) BREAKING: Wema Sepetu aachiwa huru na mahakama, Wakili wake awachana wasanii juu ya matumizi ya madawa (+video) Wakili wa Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Wema Sepetu, Alberto Msando amesema kuwa tayari mteja wake ameshalipa faini ya milioni 2 na ameshakuwa mtu huru. Hii ni baada ya asubuhi ya leo Mahakama ya Mkazi Kisutu kumhukumu msanii huyo kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini ya milioni 2 kwa kukutwa na makosa mawili ya kutumia na kuhifadhi madawa ya kulevya aina ya bangi nyumbani kwake.  Msando akiongea na waandishi wa habari mapema mchana wa leo Julai 20, 2018 nje ya mahakama baada ya hukumu hiyo kutolewa, amesema kuwa huu ni muda kwa wasanii wote kujitathmini kwani wengi wao wamekuwa wakitumia madawa ya kulevya jambo ambalo linaua vipaji vyao na kuharibu jamii kwa ujumla.

Wednesday, July 18, 2018

ZAIDI YA NUSU YA BIDHAA KATIKA SOKO LA NCHI YA UGANDA NI FEKI

Shirika la Viwango nchini Uganda (UNBS) limesema kuwa limebaini zaidi ya nusu ya bidhaa zilizo kwenye soko la nchi hiyo ni feki au viko chini ya kiwango. Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na shirika hilo mwezi Februari, umebaini kuwa takribani asilimia 54 ya bidhaa zilizoko kwenye soko la nchi hiyo hazikukidhi kiwango kilichowekwa, hivyo kuwa katika hatari zaidi ya kuwa feki. Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji Msaidizi wa Ukidhi wa Sheria – UNBS, Paul Musimami amesema kuwa asilimia hizo zimeshuka kutoka asilimia 80 iliyokuwepo miaka mitano iliyopita. Amesema kupungua kwa asimilia za bidhaa feki kumetokana na jitihada za Shirika hilo kwa kushirikiana na wadau wake. “Utafiti wetu uliofanywa Februari umebaini kuwa zaidi ya asilimia 54 ya bidhaa zilizoko sokoni hazijakidhi viwango. Kwa bahati mbaya sehemu kubwa ya bidhaa hizi ni zile zilizotengenezwa hapa nyumbani,” alisema Musimami. “Tumezuia bidhaa nyingi zilizokuwa zinaingia na ambazo zilikuwa kwenye mpango wa kuingizwa nchini kwa kutumia program ya uthibitishaji,” aliongeza. Vichanga Mapacha wafa kwa kuchomwa hospitalini Kwa mujibu wa ripoti ya Standard Bank Group, bidhaa zisizokidhi viwango nchini humo ni tatizo kubwa linalokabili uchumi likiigharimu nchi hiyo zaidi ya UGS 1 trilioni. Video: Bajeti ya upinzani kaa la moto, Mradi mpya wa maji wasomba vigogo Dawasa Musimami alieleza kuwa sehemu kubwa ya bidhaa hizo ni vifaa vya umeme, samani na chakula. Pia, alitaja vifaa vya maliwatoni pamoja na baadhi ya vipodozi.

Tuesday, July 17, 2018

WASTAAFU KULIPWA

 MENU NYUMBANI HABARI BURUDANI MICHEZO SIASA ZETU MAGAZETI ZAIDI  HABARI Wastaafu kabla ya 1999 kuanza kulipwa 1 min ago Comments Off on Wastaafu kabla ya 1999 kuanza kulipwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali inaendelea kufanya uchambuzi wa kubaini watumishi wote waliostaafu kabla ya 1999 ambao walikuwa wakichangia katika mifuko ya hifadhi ya Jamii ili waweze kulipwa madai yao ambapo mpaka sasa ni shilingi Bilioni 150 zimeshalipwa. Akizungumza na watumishi wa Chama cha Walimu Tanzania CWT kwa niaba ya Waziri Mhagama, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge kazi ajira na Vijana, Anthony Mavunde amesema ni dhamara ya Serikali kuhakikisha wastaafu wote wakiwemo walimu wanalipwa madai yao. Kwa upande wake Rais wa Chama cha Walimu Tanzania CWT, Leah Ulaya amesema changamoto kubwa wanayokabiliwa nayo ni baadhi ya vyama vinavyopingana na CWT kuleta mgogoro ndani ya chama hali inayofanya wanachama kushindwa kupata haki zao. Video: Nape aitega Serikali, CCM yaandika historia mpya Video: Rais Magufuli afungua Mkutano wa Dunia wa Vyama vya Siasa Naye katibu Mkuu wa CWT Taifa Mwalimu Deus Seif amesema kuwa walimu wanakabiliwa na Changamoto mbalimbali ambazo zinapelekea baadhi ya walimu kutotekeleza majukumu yao vyema. Hivyo wameiomba Serikali kuipa kipaumbele kada hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

MBAPE ATOA MSAADA FEDHA ZOTE ALIZOPATA KOMBE LA DUNIA

Kylian Mbappe atoa msaada fedha zote alizokusanya kombe la Dunia  Mchezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa, Kylian Mbappe ameonyesha moyo wa kipekee baada ya kutoa msaada fedha zote alizopata kwenye michinuano ya kombe la dunia dola 550,000 sawa na bilioni 1.2 za Kitanzania kwa kituo kinachotoa huduma ya michezo kwa watoto wenye ulemavu.Mbappe mwenye umri wa miaka 19 ametoa kiasi hicho cha dola za Kimarekani 550,000 ambazo zinatokana na posho pamoja na 'bonus' ya ushindi wa kombe la dunia mwaka huu 2018. Mchezaji huyo amefunga jumla ya mabao manne kwenye michuano hiyo akiitumikia timu yake ya taifa ya Ufaransa ametoa fedha hizo kwenye kituo cha Premiers de Cordee kinacho husika na kutoa bure huduma za michezo kwa watoto wasio na uwezo wa kumudu gharama pamoja na wanamichezo watoto wenye ulemavu. Kwa mujibu wa kituo cha habari cha L'Equipe kutoka nchini Ufaransa kimeeleza kuwa Mbappe hajabakiza hata kiasi kidogo cha fedha hiyo aliyopata kwenye kombe la dunia ambayo ni dola 22,500 kwa michezo iliyoshiriki timu ya Ufaransa na dola za Kimarekani 350,000 kama 'bonus' baada ya Les Bleus kushinda taji baada ya kuifunga Croatia jumla ya mabao 4 - 2.

MANENO YA RONALDO BAADA YA KUTUA JUVENTUS

Haya ndio maneno ya Ronaldo baada ya kutambulishwa Juventus Mchezaji mpya wa Juventus na timu ya taifa ya Ureno, Crisstiano Ronaldo jana ameweza kutambulishwa rasmi katika klabu hiyo na kuchukuliwa vipimo vya kiafya.Baadhi ya kauli alizozitoa mshambuliaji huyo wakati anazungumza na waandishi zimetafsiriwa tofauti na wadau mbalimbali wa michezo. "Mimi ni tofauti na wachezaji wengine wote ambao wanafikiri kazi yao iko juu ya umri wangu," alisema Ronaldo. Aliongeza, "Ninataka kuonyesha kwamba mimi si kama wengine, mimi ni tofauti, ni wakati mzuri sana kwangu na klabu kwa sababu mimi sina miaka 23, bali nina miaka 33. Umri wangu sio tatizo sana najisikia vizuri sana,najisikia kuhamasika, na nina furaha,"Mshambuliaji huyo aliyenunuliwa kwa kitita cha Euro mil 100 amesema atajumuika kwenye mazoezi na wachezaji wenzake wa timu hiyo Julai 30 mwaka huu. Ronaldo amefanikiwa kufunga magoli 450 katika klabu ya Real Madrid kwa muda wa misimu 9 huku akiisaidia kutwaa mataji 15 mataji manne ya UEFA na mawili ya Laliga,huku akichukua tuzo ya mchezaji bora Duniani Ballon d or mara tano.

MREMBO WA KIRUSI ANASWA KWA KUNYAPIA NYAPIA MAMBO YA MAREKANI

Serikali ya Marekani imemfungulia mashtaka mrembo wa Urusi mwenye umri wa miaka 29 kwa tuhuma za kufanya upelelezi na kuingilia mifumo ya siasa kwa lengo la kuivuruga nchi hiyo. Mrembo huyo aliyetajwa kwa jina la Maria Butina amedaiwa kutengeneza uhusiano mzuri na kufanya kazi kwa karibu na chama cha Republican na kwamba amekuwa mwanaharakati wa kutetea haki za kumiliki silaha, kwa mujibu wa BBC. Maria anatuhumiwa kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na ofisi ya Mueller, akiwasiliana na baadhi ya maafisa waandamizi wa Marekani. Hata hivyo, Mwanasheria anayemtetea Butina, Robert Driscoll amekanusha tuhuma hizo na kudai kuwa mteja wake sio wakala wa kijasusi wa Urusi bali ni mwanafunzi wa wa Chuo Kikuu anayechukua masomo ya Mahusiano ya Kimataifa ambaye anataka kutumia Shahada yake katika masuala ya biashara za kimataifa. Aliongeza kuwa mteja wake hajawahi kujaribu kuwashawishi watu wa aina yoyote kuzifuata au kuzipinga sheria na sera za Marekani na kwamba amekuwa akishirikiana kwa ukaribu na maafisa wa Serikali kuhusu tuhuma zinazomkabili. Habari kubwa katika Magazeti ya Tanzania leo Julai 17, 2018 Butina ambaye anaishi Washington, Marekani alikamatwa Jumapili iliyopita na ameendelea kushikiliwa mahabusu akisubiri kupandishwa kizimbani Jumatano wiki hii, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Haki (DOJ). Video: Fahamu migahawa 6 inayotoa huduma za ajabu duniani Taarifa za kukamatwa kwa msichana huyo zimewekwa wazi muda mfupi baada ya Rais Donald Trump kukutana na Rais wa Urusi, Vladimir Putin. Katika mkutano huo Trump aliitetea Urusi kuhusu tuhuma za kuingilia uchaguzi wa mwaka 2016. FBI wameeleza kuwa baada ya kumfuatilia, walibaini kuwa alikuwa anafanya kazi ya kushawishi kukubalika kwa Urusi pia miongoni mwa maafisa waandamizi wa Marekani na kuanzisha taasisi za kiharakati kinyume na kibali chake cha kuingia nchini humo. Alianza kundi la kutetea haki za kumiliki silaha aliloliita ‘Bear Arms’ na pia alikuwa na uhusiano wa karibu na National Riffle Association.  Maria Butina Aidha, ripoti ya FBI imesema kuwa walibaini Butina alikuwa anaripoti maendeleo ya kazi yake kwa Serikali ya Urusi kupitia jumbe za moja kw amoja za Twitter (Twitter direct messages). Mrembo huyo ambaye asili yake ni Serbia, anadaiwa kuwa alihudhuria pia mikutano ya Trump na kupata nafasi ya kumuuliza maswali, akitaka kujua msimamo wake kuhusu uhusiano wa Marekani na Urusi.

Monday, July 16, 2018

RAIA INDONESIA WALIPA KISASI

Kundi la wanakijiji nchini Indonesia wamefanikiwa kuwaua mamba wapatao 300 kwenye makao makuu ya wanyama katika mkoa was West Papua.

Mauaji hayo yalikuwa ni yakulipiza kisasi cha kifo cha mwanaume mmoja aliyeuawa katika eneo hilo.

Maafisa wa polisi wanasema hawakuweza kuzuia mauaji hayo ila watafungua mashtaka dhidi ya waliohusika katika mauaji hayo.
Kwa makosa kama haya nchini Indonesia adhabu yake ni pamoja na kifungo.

Wednesday, July 11, 2018

SIMBA SC YATINGA FINALI

Simba sc imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya Kagame Super Cup.Simba sc wamelazimika kusubiri hadi dakika ya (41) ambapo mchezaji mwenye asili ya kinyarwanda Meddie Kagere amefanikiwa kukwamisha mpira nyavuni.

Monday, July 9, 2018

HATUA MOJA HUANZISHA NYINGINE

Katibu mkuu kiongozi,John Kijazi amesema mpaka mwishoni mwa mwaka huu serikali itakuwa imeagiza ndege nyingine mbili aina ya Bombardier hivyo kufanya kuwa na ndege sita za kisasa.

"Mwito wangu kwa ATCL,watunze ndege hizi na kuhakikisha wanazihudumia vizuri na kuendesha kibiashara.kwa kufanya hivyo serikali itakuwa na uwezo wa kununua ndege nyingine."amesema

Tuesday, June 26, 2018

YAMETIMIA

Klabu ya Simba ya jijini Dar es salaam imefanikiwa kumsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Gor Mahia ya nchini Kenya.

Mshambuliaji huyu raia wa Rwanda amesajiliwa kwa kitita cha shilingi ml. 110.

DEAL DONE

Kiungo mbelgiji Radja Nainggolan aliyekuwa akikipiga katika klabu ya AS Roma amejiunga na klabu ya Inter Milan kwa Euro 21

Monday, June 25, 2018

PACHA WALIOUNGANA KUPELEKWA SAUDI ARABIA

Mfalme wa Saudi Arabia amekubali pacha walioungana,Marines na Anisia Beatus kupelekwa nchini humo kuangalia uwezekano wa kuwatenganisha mapacha hao walioungana sehemu ya kifuani.

Mapacha hao wamelazwa katika hospitali ya Muhimbili (MNH) tangu februari wakipatiwa matibabu.

Thursday, June 7, 2018

CHINI YA KAPETI

Klabu ya Singida United imetibitisha uwezekano mdogo wa kuikosa huduma ya mchezaji wake Deus Kaseke.
Kwa mujibu wa msemaji wake,Festo Sanga amesema,"Kuna uwezekano mdogo wa kupata huduma ya mchezaji huyo kutokana klabu moja ya Afrika kusini kuhitaji huduma yake".

MWENDELEZO WA SPORTPESA SUPER

KIKOSI CHA SIMBA VS KK HOMEBOYZ

1.Aishi Manula
2.Shomari Kapombe
3.Mohamed Zimbwe
4.Paul Bukaba
5.Erasto Nyoni
6.Jonasi Mkude
7.Shiza Kichuya
8.Muzamiru Yassin
9.Mohammed Rashid
10.Rashid Juma
11.Haruna Niyonzima
        
           SUB.
1.Salim Ally
2.Ally Shomari
3.Yusufu Mlipili
4.Mohamed Ibrahim
5.Marcel Kaheza
6.Adamu Salamba

Wednesday, June 6, 2018

KAZI YA KUENEZA WOKOVU NA CHANGAMOTO ZAKE

Ethiopia
Mchungaji mmoja kwa Majina Docho Eshete ameuawa kwa kushambuliwa na mamba akiwa anawafanyia ubatizo waumini wapya ziwani

Hakuna kupoa

Ratiba kamili ya CECAFA-KAGAME

Habari mpya

Ajali mbaya imetokea mkoani Kigoma Kahabwa Kata ya Gungu.
Ajali hiyo imehusisha treni ya mizigo name basi lifanyalo safari za Kigoma -Tabora

MATOKEO YA UPONYAJI UGONJWA WA UKIMWI

Mgonjwa aliyekuwa na virusi vya HIV atangazwa kutokuwa tena na virusi hivyo Watafiti nchini Uingereza wamebainisha kwamba raia mmoja wa taif...