Kundi la wanakijiji nchini Indonesia wamefanikiwa kuwaua mamba wapatao 300 kwenye makao makuu ya wanyama katika mkoa was West Papua.
Mauaji hayo yalikuwa ni yakulipiza kisasi cha kifo cha mwanaume mmoja aliyeuawa katika eneo hilo.
Maafisa wa polisi wanasema hawakuweza kuzuia mauaji hayo ila watafungua mashtaka dhidi ya waliohusika katika mauaji hayo.
Kwa makosa kama haya nchini Indonesia adhabu yake ni pamoja na kifungo.
No comments:
Post a Comment